ERB YOUTH ENGINEERING FORUM

SERIKALI YAWEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA WAHANDISI WAZAWA
Serikali imesema kuwa imeandaa mkakati maalum wa kutoa fursa za ajira na kutengeneza mazingira wezeshi kwa wahandisi wazawa kutekeleza miradi mikubwa ya maendeleo nchini ili kuwainua kichumi na kuleta maendeleo nchini.
Ameyasema hayo, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mheshimiwa Patrobas Katambi leo, Septemba 3, 2024 wakati akifungua Jukwaa la Wahandisi Vijana jijini Dar es Salaam lililobebwa na kauli mbiu isemayo “Kuwainua Vijana katika safari yao ya Taaluma na Biashara” ambalo limeratibiwa na Bodi ya Usajili wa Wahandisi (ERB).